
Na Mapuli Kitina Misalaba
Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yanayoendelea katika
uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
yameendelea kushika kasi ambapo mchezo wa leo Machi 21, 2026 uliwakutanisha
MAHEMBE FC dhidi ya MAWEMIRU katika pambano lililovutia mashabiki waliojitokeza
kushuhudia burudani ya soka.
Katika mchezo huo, MAHEMBE FC imefanikiwa kuibuka na
ushindi dhidi ya MAWEMIRU baada ya kuonesha kiwango kizuri ndani ya dakika 90
za mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa kuanzia kipindi cha kwanza hadi
mwisho wa mchezo.
Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na
Bwana Paul Daud Augustino kupitia udhamini na wadau mbalimbali ikiwemo Lushu
Foundation kwa lengo la kuibua vipaji vya vijana, kuimarisha mshikamano wa
jamii pamoja na kuendeleza michezo katika Mkoa wa Shinyanga.
Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa
Shinyanga Said Mankiligo amezitaka timu pamoja na vijana wanaoshiriki
mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 kuendelea kuzingatia sheria, kanuni na
taratibu zilizowekwa ili kuhakikisha mashindano hayo yanaendelea kwa amani na
ushindani wa haki.
Mankiligo amesema nidhamu ni msingi mkubwa wa
mafanikio katika michezo hivyo wachezaji wanapaswa kuheshimu waamuzi, viongozi
wa timu pamoja na mashabiki wakati wote wa mashindano hayo.
Aidha amewahimiza vijana kutumia mashindano hayo kama
sehemu ya kuonesha vipaji vyao kwa njia ya nidhamu, mshikamano na kujituma ili
waweze kuonekana na kupata nafasi katika timu mbalimbali za ngazi ya juu.
Baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya Mashindano
Sambayi Jilya ametangaza ratiba ya mechi ya derby kesho ambapo timu ya
NYANDOLWA itashuka dimbani kumenyana na BAJAJ FC katika mchezo unaotarajiwa
kuwa na ushindani mkubwa ndani ya uwanja wa Mwabenda.
Aidha amewakaribisha wananchi na wadau wa michezo kuendelea kujitokeza kwa wingi kushuhudia michezo hiyo ambayo imeendelea kuwa jukwaa muhimu la kuibua vipaji vya vijana kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Shinyanga.
Timu ya Mahembe FC
Timu ya Mawemiru FC.
Waamuzi wa mechi.
Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Shinyanga Said Mankiligo akizungumza na wachezaji na viongozi wa timu kuhusu umuhimu wa kuzingatia sheria na nidhamu katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026.
Mchezo ukiendelea katika uwanja wa Mwabenda huku vijana wakionesha vipaji vyao kupitia mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026.

Mchezo ukiendelea katika uwanja wa Mwabenda huku vijana wakionesha vipaji vyao kupitia mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026.
Mahembe FC baada ya kupata goli.
Sehemu ya viongozi pamoja na wadau wa michezo wakifuatilia maelekezo yaliyotolewa kwa timu zinazoshiriki mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026.SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254









Post a Comment