Na Mapuli Kitina Misalaba
Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa
Shinyanga Said Mankiligo ameendelea kumpongeza mwandaaji wa mashindano ya
NIACHEKONA CUP 2026 Bwana Paul Daud Augustino kwa juhudi anazoendelea kuzifanya
katika kuinua vipaji vya vijana kupitia michezo.
Akizungumza leo Mei 23, 2026 katika muendelezo wa
mashindano hayo yanayoendelea kwenye uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa,
Mankiligo amesema ligi hiyo imekuwa na mchango mkubwa katika kuwaunganisha
vijana pamoja na kujenga mahusiano mema ndani ya jamii.
“Naendelea kumpongeza mwandaaji wa
mashindano haya kwa kazi kubwa anayofanya. Mashindano haya yanajenga undugu,
yanaleta mahusiano lakini pia ni ajira kwa vijana wetu,”
amesema Mankiligo.
Aidha amewahimiza waamuzi wanaochezesha mashindano
hayo kuhakikisha wanatekeleza sheria 17 za mchezo wa mpira wa miguu kwa usahihi
ili kuendelea kudumisha haki, amani pamoja na ushindani wa kweli ndani ya
mashindano hayo.
Katika mchezo wa leo, timu ya SHILABELA imeibuka na
ushindi wa bao 1-0 dhidi ya LYABUKANDE FC mchezo ambao umekuwa na ushindani
mkubwa huku mashabiki wakifurahia burudani ya soka katika uwanja wa Mwabenda.
Baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya Mashindano
Sambayi Jilya ametangaza ratiba ya mchezo wa kesho ambapo timu ya KIMANDAGULI
itamenyana na KASHISHI katika mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa
ndani ya NIACHEKONA CUP 2026.
Mashindano hayo yameandaliwa na Bwana Paul Daud
Augustino kupitia ufadhili wa Lushu Foundation kwa lengo la kuibua vipaji vya
vijana, kuimarisha mshikamano wa jamii pamoja na kukuza michezo katika Mkoa wa
Shinyanga.
Kwa huduma za ushereheshaji wa shughuli mbalimbali,
matangazo pamoja na burudani unaweza kuwasiliana na MC NIACHEKONA kupitia namba
0757 267 738.

Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Shinyanga Said Mankiligo na viongozi mbalimbali wakifuatilia mechi.
Mashabiki wakifuatilia mchezo wa SHILABELA dhidi ya LYABUKANDE FC katika uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa.

Mashabiki wakifuatilia mchezo wa SHILABELA dhidi ya LYABUKANDE FC katika uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa.

Mashabiki wakifuatilia mchezo wa SHILABELA dhidi ya LYABUKANDE FC katika uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa.

Mashabiki wakifuatilia mchezo wa SHILABELA dhidi ya LYABUKANDE FC katika uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa.

Mashabiki wakifuatilia mchezo wa SHILABELA dhidi ya LYABUKANDE FC katika uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa.

Mashabiki wakifuatilia mchezo wa SHILABELA dhidi ya LYABUKANDE FCSHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
katika uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa.



































Post a Comment