" NYUNDO FC NA NZOZA ZAGAWANA POINTI NIACHEKONA CUP 2026

NYUNDO FC NA NZOZA ZAGAWANA POINTI NIACHEKONA CUP 2026

Na Mapuli Kitina Misalaba


Ligi ya NIACHEKONA CUP 2026 inayoendelea katika uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga imeendelea kushika kasi ambapo mchezo wa leo kati ya NYUNDO FC na NZOZA umemalizika kwa sare ya bao 1-1 katika pambano lililokuwa na ushindani mkubwa na kuvutia mashabiki wengi waliojitokeza kushuhudia burudani ya soka.

Mashindano hayo yanayoendelea kuibua vipaji vya vijana kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Shinyanga yameendelea kuwa kivutio kikubwa kwa wadau wa michezo kutokana na ushindani wa timu pamoja na mwitikio wa wananchi.

Baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya Mashindano Sambayi Jilya ametangaza matokeo ya mchezo wa leo pamoja na kusoma ratiba ya mechi ya kesho ambapo timu ya MAHEMBE itamenyana na MAWEMIRU katika mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa ndani ya uwanja wa Mwabenda.

Akiendelea kuzungumza, Sambayi amewakaribisha wananchi na wadau wa michezo kujitokeza kwa wingi kushuhudia michezo hiyo ambayo imeendelea kuwa jukwaa la kuibua vipaji vya vijana kutoka maeneo mbalimbali.

Kwa upande wake mdau wa michezo Joseph Mbogo amepongeza jitihada zinazofanywa na mwandaaji wa mashindano hayo Bwana Paul Daud Augustino kwa namna anavyoendelea kutumia michezo kuwaunganisha vijana pamoja na kuibua vipaji vyao.

Mbogo amesema NIACHEKONA CUP imekuwa chachu kubwa ya maendeleo ya michezo katika kata ya Solwa na Wilaya ya Shinyanga kwa ujumla kutokana na kuwapa vijana nafasi ya kuonesha uwezo wao mbele ya wadau mbalimbali wa soka.

Aidha ameomba serikali kuendelea kumuunga mkono MC NIACHEKONA katika juhudi zake za kuinua vipaji vya vijana kupitia michezo huku akiiomba pia kuangalia nafasi inayoweza kumfaa katika sekta ya michezo iwe ndani ya Wizara ya Michezo au Idara ya Michezo katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kutokana na mchango wake mkubwa anaouonesha kwa jamii kupitia michezo.

Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yanaendelea kila siku kuanzia saa kumi jioni katika uwanja wa Mwabenda huku yakishirikisha jumla ya timu 22 kutoka maeneo mbalimbali ikiwemo Mkoa wa Mwanza, Geita, Kahama, Manispaa ya Shinyanga pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Kwa huduma za ushereheshaji wa shughuli mbalimbali, matangazo, burudani, michezo, sherehe za kijamii na matukio tofauti wasiliana na MC NIACHEKONA kupitia namba 0757 267 738.

Nyundo FC kabla ya mechi.


 Mchezo ukiendelea katika uwanja wa Mwabenda ambapo NYUNDO FC na NZOZA ziligawana pointi baada ya kutoka sare ya bao 1-1.

Post a Comment

Previous Post Next Post