Na Edington Mukiza Ezron, Misalaba Media
Baadhi ya wananchi katika Manispaa ya Shinyanga
wamewataka viongozi wa serikali pamoja na watumishi wa taasisi mbalimbali kuwa
waadilifu na kuacha kujihusisha na vitendo vya rushwa ili kulinda haki za
wananchi na kuchochea maendeleo ya jamii.
Wakizungumza na Misalaba Media kwa nyakati tofauti Mei
8, 2026, wananchi hao wamesema vitendo vya rushwa vinaendelea kuathiri utoaji
wa huduma katika taasisi mbalimbali na kusababisha wananchi wengi kukosa haki
zao za msingi.
Mmoja wa wananchi hao, William Muhangwa, amesema
baadhi ya viongozi na watumishi wa taasisi za umma wamekuwa wakijihusisha na
vitendo vya rushwa vinavyowakosesha wananchi wasiokuwa na uwezo kupata huduma
kwa haki na kwa wakati.
Ameongeza kuwa baadhi ya wananchi hulazimika kutoa
rushwa ili kuharakisha huduma kutokana na ucheleweshaji unaofanywa katika
baadhi ya ofisi na taasisi.
Aidha, wananchi hao wameeleza kuwa ukosefu wa ajira
nao umechangia kuongezeka kwa vitendo vya rushwa, kutokana na uwepo wa wahudumu
wachache wanaotoa huduma kwa idadi kubwa ya wananchi, hali inayosababisha
mlundikano wa wahitaji wa huduma.
Pia wamebainisha kuwa rushwa inazorotesha maendeleo ya
jamii kwa kuathiri utekelezaji wa miradi ya maendeleo, huduma za kijamii pamoja
na haki za binadamu, hivyo jamii inapaswa kushirikiana kupinga vitendo hivyo
kwa manufaa ya taifa.
Wameongeza kuwa waajiri wanapaswa kuwasisitiza
watumishi wa taasisi mbalimbali kuzingatia maadili ya kazi na kuacha kupokea
rushwa ili kulinda haki za wananchi pamoja na heshima ya taasisi zao.
Hata hivyo, wananchi hao wameitaka Taasisi ya Kuzuia
na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuendelea kuchukua hatua kali za kisheria
dhidi ya watakaobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa, sambamba na kuongeza
elimu kwa jamii kuhusu madhara ya rushwa na umuhimu wa kupambana nayo.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment