Diwani wa Kata ya Mwawaza Manispaa ya Shinyanga, Edwin
Charles Washa, leo amefanya mkutano wa hadhara na wananchi wa kata hiyo kwa
lengo la kuwashukuru kwa imani waliyoonyesha kwa kumchagua kuwa mwakilishi wao,
pamoja na kusikiliza na kutafuta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali
zinazowakabili.
Mkutano huo ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali,
akiwemo Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Shinyanga mjini Samwel Jackson.
Katika mkutano huo, wananchi walipata fursa ya
kuwasilisha maoni, kero na mapendekezo yao kuhusu huduma mbalimbali za kijamii
na maendeleo, huku viongozi waliokuwepo wakitoa majibu na ufafanuzi wa masuala
yaliyoibuliwa.
Akizungumza katika mkutano huo, Diwani Edwin Charles
Washa aliwashukuru wananchi kwa ushirikiano wanaoendelea kuonyesha na kuahidi
kuendelea kusimamia na kutetea maslahi ya wananchi wa Kata ya Mwawaza kwa
kushirikiana na viongozi wa serikali na wadau wengine wa maendeleo.
Aidha, aliwahimiza wananchi kuendelea kushiriki katika
shughuli za maendeleo na kudumisha ushirikiano ili kuharakisha maendeleo ya
kata hiyo na kuboresha huduma zinazotolewa kwa wananchi.
Viongozi wengine ambao wamehudhuria mkutano huo ni Diwani
wa Viti Maalumu tarafa ya Shinyanga mjini, Mwanahamisi Kazoba Mtendaji wa Kata
ya Mwawaza, Naomi Stanley Kimaro Afisa Elimu wa Kata hiyo, Elizabeth Mboje
Samweli Afisa Huduma kwa Wateja Masaka Kabesha, Mhandisi wa TARURA Eng. Kulwa
Maige, pamoja na Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Saidi Bwaga.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254













Post a Comment