Na Mapuli
Kitina Misalaba
Timu ya Duara
FC imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya mashindano ya NIACHEKONA CUP
2026 baada ya kuibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Mawemiru FC katika mchezo
wa robo fainali uliochezwa leo Juni 14, 2026 katika Uwanja wa Mwabenda, Kata ya
Solwa.
Bao pekee la
ushindi kwa Duara FC lilifungwa na Neno Michael katika kipindi cha kwanza cha
mchezo huo, bao ambalo lilidumu hadi dakika 90 na kuipa timu yake tiketi ya
kusonga mbele katika hatua inayofuata ya mashindano hayo.
Mchezo huo
uliokuwa na ushindani mkubwa uliwashuhudia wachezaji wa Mawemiru FC wakifanya
juhudi za kutafuta bao la kusawazisha, lakini walishindwa kuvunja ngome ya
Duara FC iliyokuwa imara hadi mwisho wa mchezo.
Kwa matokeo
hayo, safari ya Mawemiru FC imehitimishwa katika hatua ya robo fainali, huku
Duara FC ikijiweka katika nafasi nzuri ya kuwania ubingwa wa mwaka huu.
Baada ya
ushindi huo, nahodha pamoja na kocha wa Duara FC wametuma ujumbe kwa wapinzani
wao wa hatua ya nusu fainali, Ufukunyungu FC, wakisema kuwa timu yao ipo tayari
kwa pambano hilo na wana imani kubwa ya kupata ushindi utakaowapeleka moja kwa
moja katika hatua ya fainali.
Kwa mujibu
wa ratiba ya mashindano hayo, nusu fainali ya kwanza itawakutanisha Ufukunyungu
FC dhidi ya Duara FC katika mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa
kutokana na kiwango walichoonyesha timu hizo katika hatua zilizopita.
Akizungumza
baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya Mashindano ya NIACHEKONA CUP, Sambayi
Jilya, ametangaza ratiba ya mchezo wa kesho ambapo Nyandolwa FC kutoka Kata ya
Mwenge Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga itamenyana na Bulige FC kutoka
Halmashauri ya Msalala Wilaya ya Kahama katika mchezo mwingine wa robo fainali.
Sambayi
Jilya amewahimiza wananchi na wadau wa michezo kuendelea kujitokeza kwa wingi
katika Uwanja wa Mwabenda kushuhudia michezo iliyobaki ya mashindano hayo.
Mgeni maalum
wa mchezo wa leo alikuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa
Shinyanga, Said Mankiligo, ambaye aliambatana na baadhi ya wachezaji wa zamani
waliowahi kuandika historia ya soka katika Kijiji cha Mwabenda.
Mankiligo
amempongeza mwandaaji wa NIACHEKONA CUP 2026, Paul Daud Augustino maarufu MC
NIACHEKONA, kwa kuendelea kuibua vipaji vya vijana kupitia michezo.
Aidha,
amezihimiza timu zinazoshiriki Ligi Daraja la Kwanza, Ligi ya Mabingwa wa Mikoa
na mashindano mengine makubwa kujitokeza kufuatilia michezo ya NIACHEKONA CUP
ili kupata fursa ya kusajili wachezaji wenye vipaji wanaoshiriki mashindano
hayo.
Amesema
NIACHEKONA CUP imeendelea kuwa jukwaa muhimu la kuibua vipaji vya vijana na
kwamba kuna wachezaji wengi wenye uwezo mkubwa wanaoweza kupata nafasi katika
timu mbalimbali kwa gharama nafuu.
Mashindano
ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na Paul Daud Augustino maarufu MC
NIACHEKONA kwa ufadhili wa Shirika la Lushu Foundation, yakilenga kuibua vipaji
vya vijana, kukuza michezo na kuimarisha mshikamano wa jamii.
Kwa huduma
za MC, matangazo na ushereheshaji wa matukio mbalimbali, wasiliana na MC
NIACHEKONA kupitia namba 0757 267 738.
Kikosi cha (Manonga) Duara FC.
Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Shinyanga, Said Mankiligo, akisalimiana na wachezaji kabla ya kuanza kwa mchezo wa robo fainali katika NIACHEKONA CUP 2026.
Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Shinyanga, Said Mankiligo, akisalimiana na wachezaji kabla ya kuanza kwa mchezo wa robo fainali katika NIACHEKONA CUP 2026.
Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Shinyanga, Said Mankiligo, akisalimiana na wachezaji kabla ya kuanza kwa mchezo wa robo fainali katika NIACHEKONA CUP 2026.
Wachezaji wa Duara FC na Mawemiru FC wakionyesha ushindani mkubwa katika mchezo wa robo fainali ya NIACHEKONA CUP 2026.
Mchezo mkali ukiendelea Uwanja wa Mwabenda huku timu zote zikisaka nafasi ya kutinga hatua ya nusu fainali.
Burudani ya soka ikiendelea kushuhudiwa katika pambano la robo fainali kati ya Duara FC na Mawemiru FC.
Viongozi wa mashindano na wadau wa michezo wakifuatilia kwa karibu mchezo wa leo katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026.
Viongozi wa mashindano na wadau wa michezo wakishuhudia ushindani mkubwa wa robo fainali katika Uwanja wa Mwabenda.
Viongozi wa mashindano na wadau wa michezo wakifuatilia mwenendo wa mchezo huo uliovutia mashabiki wengi.
Mashabiki na wananchi waliojitokeza kwa wingi wakifuatilia mchezo wa robo fainali katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026.
Mashabiki na wananchi waliojitokeza kwa wingi wakifuatilia mchezo wa robo fainali katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026.
Mashabiki na wananchi waliojitokeza kwa wingi wakifuatilia mchezo wa robo fainali katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026.
Wananchi kutoka maeneo mbalimbali wakifuatilia kwa hamasa kubwa mchezo wa Duara FC dhidi ya Mawemiru FC.
Wananchi kutoka maeneo mbalimbali wakifuatilia kwa hamasa kubwa mchezo wa Duara FC dhidi ya Mawemiru FC.





























































Post a Comment