Na Mapuli Kitina Misalaba
Maajabu yameendelea kushuhudiwa katika mashindano ya NIACHEKONA
CUP 2026 baada ya Kashishi FC kumuondoa kigogo mwingine, Shilabela FC, na
kufanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali.
Kashishi FC, ambayo hivi karibuni ilimuondoa bingwa
mtetezi wa mashindano hayo Sangu FC, leo Juni 16, 2026 imeendelea kuonyesha
ubora wake baada ya kuitoa Shilabela FC, timu iliyowahi kufika fainali ya msimu
wa 2024/2025 dhidi ya Sangu FC.
Mchezo huo wa robo fainali uliochezwa katika Uwanja wa
Mwabenda, Kata ya Solwa, umemalizika kwa sare ya bila kufungana ndani ya dakika
90 za kawaida, hali iliyozilazimu timu hizo kwenda katika hatua ya mikwaju ya
penati kutafuta mshindi.
Katika mikwaju hiyo ya penati, Kashishi FC ilionyesha
utulivu mkubwa na kufanikiwa kupata penati 4 kwa 3, matokeo yaliyoihakikishia
nafasi ya kutinga hatua ya nusu fainali huku safari ya Shilabela FC ikifikia
tamati.
Kwa ushindi huo, Kashishi FC imejiwekea rekodi ya kuwa
miongoni mwa timu zilizofanya makubwa zaidi katika mashindano ya mwaka huu
baada ya kuwaondoa vigogo wawili mfululizo waliokuwa wakipewa nafasi kubwa ya
kufika fainali.
Hatua ya nusu fainali sasa itawakutanisha Kashishi FC
dhidi ya Bulige FC katika mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana
na kiwango walichoonyesha timu hizo katika hatua zilizopita.
Akizungumza baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya
Mashindano ya NIACHEKONA CUP, Sambayi Jilya, amesema kuwa kesho Jumatano
kutakuwa na mapumziko ili kutoa nafasi kwa maandalizi ya hatua ya nusu fainali.
Amesema mchezo wa kwanza wa nusu fainali utachezwa Alhamisi,
Juni 18, ambapo Ufukunyungu FC itamenyana na Duara FC, huku mchezo wa pili wa
nusu fainali ukiwakutanisha Bulige FC na Kashishi FC siku ya Juni 19.
Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na Paul
Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa Shirika la Lushu
Foundation, yakilenga kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo na kuimarisha
mshikamano wa jamii.
Kwa huduma za MC, matangazo na ushereheshaji wa
matukio mbalimbali, wasiliana na MC NIACHEKONA kupitia namba 0757 267 738.
Kikosi cha Shilabela FC.
Wachezaji wa Kashishi FC na Shilabela FC wakipambana kusaka nafasi ya kutinga hatua ya nusu fainali.
Mchezo wa robo fainali ukiendelea kwa ushindani mkubwa mbele ya mamia ya mashabiki katika Uwanja wa Mwabenda.
Wachezaji wa Kashishi FC na Shilabela FC wakipambana kusaka nafasi ya kutinga hatua ya nusu fainali.
Wachezaji wa timu zote mbili wakionesha kiwango cha juu katika pambano la robo fainali ya NIACHEKONA CUP 2026.
Viongozi wa mashindano na wadau wa michezo wakifuatilia mchezo wa robo fainali ya mwisho wa NIACHEKONA CUP 2026.
Viongozi wa mashindano na wadau wa michezo wakifuatilia mchezo wa robo fainali ya mwisho wa NIACHEKONA CUP 2026.
Mashabiki na wananchi waliojitokeza kwa wingi kushuhudia mchezo wa robo fainali ya mwisho katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026.
Wananchi kutoka maeneo mbalimbali wakifuatilia kwa makini pambano la Kashishi FC dhidi ya Shilabela FC.
Wananchi kutoka maeneo mbalimbali wakifuatilia kwa makini pambano la Kashishi FC dhidi ya Shilabela FC.
Mashabiki na wananchi waliojitokeza kwa wingi kushuhudia mchezo wa robo fainali ya mwisho katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026.
Mashabiki na wananchi waliojitokeza kwa wingi kushuhudia mchezo wa robo fainali ya mwisho katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026.SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254






























Post a Comment