Na Mapuli Kitina Misalaba
Mkurugenzi wa mashindano ya NIACHEKONA CUP, Paul Daud
Augustino maarufu MC NIACHEKONA, amewashukuru Watanzania, wadau wa michezo na
timu zote zilizoshiriki mashindano hayo kwa kuonyesha ushindani wa hali ya juu
pamoja na nidhamu tangu kuanza kwa michuano hiyo hadi kufikia hatua ya fainali.
Akizungumza baada ya kukamilika kwa michezo ya nusu
fainali, MC NIACHEKONA amesema timu zilizofanikiwa kutinga fainali ni Ufukunyungu
FC kutoka Manispaa ya Shinyanga na Kashishi FC kutoka Kata ya Solwa, huku
akieleza kufurahishwa na kiwango na nidhamu iliyoonyeshwa na washiriki wa
mashindano hayo.
"Ninawashukuru Watanzania wote na
timu zote zilizoshiriki katika mashindano haya. Mmeonyesha mpira mzuri na
nidhamu ya hali ya juu tangu tulipoanza hadi tumefikia hatua hii ya
fainali," amesema NIACHEKONA.
Ametumia nafasi hiyo kuwaalika wananchi na wadau
mbalimbali wa michezo kuhudhuria mchezo wa fainali utakaofanyika Jumanne, Juni
23, 2026, katika Uwanja wa Mwabenda, Kata ya Solwa.
Amesema siku hiyo mchezo wa kusaka mshindi wa tatu
utaanza saa nane mchana, huku saa kumi kamili kukiwa na hotuba ya mgeni rasmi
ambaye atatangazwa rasmi siku ya Jumatatu kabla ya kuanza kwa mchezo wa
fainali.
"Ninawaalika Watanzania wote
kuhudhuria fainali hii. Kutakuwa na burudani mbalimbali na shughuli nyingi za
kuvutia kwa mashabiki na wananchi wote watakaohudhuria,"
ameongeza.
MC NIACHEKONA pia amewashukuru wadau mbalimbali
waliochangia mafanikio ya mashindano hayo, akilitaja Shirika la Lushu
Foundation kwa kuendelea kuwa mdhamini mkuu wa mashindano pamoja na Misalaba
Media kwa kazi ya kuripoti na kusambaza taarifa za mashindano kwa wananchi
kupitia vyombo na mitandao ya kijamii.
Aidha, amesema yupo tayari kushirikiana na wadau wote
wa michezo wanaotaka kuendeleza vipaji na kukuza michezo nchini kutokana na
uzoefu alioupata katika kuandaa na kusimamia mashindano mbalimbali.
Kumbuka huu ni msimu wa tatau wa Mashindano ya NIACHEKONA
CUP ambayo yameandaliwa na Paul Daud
Augustino maarufu MC NIACHEKONA na kwambwa msimu huu yamefadhiliwa na Shirika
la Lushu Foundation, ikiwa lengo ni kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo na
kuimarisha mshikamano wa jamii.
Kwa huduma za MC, matangazo na ushereheshaji wa
matukio mbalimbali, wasiliana na MC NIACHEKONA kupitia namba 0757 267 738.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment