Na Mapuli Kitina Misalaba
Timu ya Ufukunyungu FC imefanikiwa kutinga hatua ya
nusu fainali ya mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 baada ya kuibuka na ushindi
wa goli 1-0 dhidi ya Songambele Mhangu FC katika mchezo wa kwanza wa robo
fainali uliochezwa leo Juni 13, 2026 katika Uwanja wa Mwabenda, Kata ya Solwa
Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.
Mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa ulimalizika
kwa Ufukunyungu FC kupata bao pekee la ushindi katika kipindi cha pili kupitia
mshambuliaji wake Said Saidi, ambaye aliandika historia ya kuipa timu yake
tiketi ya kutinga hatua inayofuata ya mashindano hayo.
Bao hilo lilidumu hadi dakika 90 za mchezo, huku
Songambele Mhangu FC ikishindwa kupata bao la kusawazisha licha ya kufanya
juhudi mbalimbali mbele ya lango la wapinzani wao.
Kwa ushindi huo, Ufukunyungu FC imefanikiwa kumuondoa
mmoja wa vigogo waliokuwa wakitajwa kuwania ubingwa wa NIACHEKONA CUP 2026.
Songambele Mhangu FC ilikuwa miongoni mwa timu zilizokuwa zikipewa nafasi kubwa
ya kufanya vizuri kutokana na historia yake nzuri katika mashindano mbalimbali
pamoja na kuwa na wadhamini waliokuwa wakiiwezesha timu hiyo.
Baada ya mchezo huo, mashabiki na wadau wa michezo
wamepongeza kiwango kilichooneshwa na timu zote mbili huku wakieleza kuwa
ushindi wa Ufukunyungu FC umeongeza ushindani katika hatua ya nusu fainali.
Akizungumza baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya
Mashindano ya NIACHEKONA CUP, Sambayi Jilya, ametangaza ratiba ya mchezo wa
kesho ambapo Duara FC itamenyana na Mawemiru FC katika mchezo mwingine wa robo
fainali utakaochezwa katika Uwanja wa Mwabenda.
Sambayi Jilya amewahimiza wananchi, mashabiki na wadau
wa michezo kuendelea kujitokeza kwa wingi kushuhudia michezo iliyosalia katika
hatua ya robo fainali.
Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na Paul
Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa Shirika la Lushu
Foundation, yakiwa na lengo la kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo na
kuimarisha mshikamano wa jamii.
Kwa huduma za MC, matangazo na usimamizi wa matukio
mbalimbali ya kijamii, wasiliana na Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA
kupitia namba 0757 267 738.
Kikosi cha Songambele Mhangu FC.
Mchezo wa robo fainali kati ya Songambele Mhangu FC na Ufukunyungu FC ukiendelea katika Uwanja wa Mwabenda.
Mchezo wa robo fainali kati ya Songambele Mhangu FC na Ufukunyungu FC ukiendelea katika Uwanja wa Mwabenda.
Viongozi wa mashindano na wadau wa michezo wakifuatilia kwa karibu mchezo wa robo fainali kwenye NIACHEKONA CUP 2026.
Mashabiki na wananchi waliojitokeza kwa wingi kushuhudia pambano la Songambele Mhangu FC dhidi ya Ufukunyungu FC.
Mashabiki na wananchi waliojitokeza kwa wingi kushuhudia pambano la Songambele Mhangu FC dhidi ya Ufukunyungu FC.
Mashabiki na wananchi waliojitokeza kwa wingi kushuhudia pambano la Songambele Mhangu FC dhidi ya Ufukunyungu FC.
Mashabiki na wananchi waliojitokeza kwa wingi kushuhudia pambano la Songambele Mhangu FC dhidi ya Ufukunyungu FC.
Mashabiki na wananchi waliojitokeza kwa wingi kushuhudia pambano la Songambele Mhangu FC dhidi ya Ufukunyungu FC.
Mashabiki na wananchi waliojitokeza kwa wingi kushuhudia pambano la Songambele Mhangu FC dhidi ya Ufukunyungu FC.SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254








































Post a Comment