" KAMANDA MAGOMI: MAENDELEO YANAHITAJI AMANI NA UZINGATIAJI WA SHERIA

KAMANDA MAGOMI: MAENDELEO YANAHITAJI AMANI NA UZINGATIAJI WA SHERIA

Na Mapuli Kitina Misalaba

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, SACP Janeth Magomi, amewahimiza wananchi kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kulinda na kudumisha amani, akisisitiza kuwa usalama ni jukumu la kila mwananchi.

Amesema kila mtu ana haki ya kufanya kazi, kuendesha biashara na kutekeleza shughuli zake za kila siku katika mazingira ya utulivu na usalama, hivyo ni muhimu kuepuka vitendo vinavyoweza kuvuruga amani.

Kuhusu masuala ya maandamano, Kamanda Magomi amesema shughuli hizo zinapaswa kufanyika kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni za nchi, huku akiwataka wananchi kutoshiriki vitendo vya uchochezi au uvunjifu wa sheria vinavyoweza kuhatarisha usalama wa watu na mali zao.

Ameongeza kuwa Jeshi la Polisi litaendelea kusimamia utekelezaji wa sheria kwa haki na weledi ili kuhakikisha Mkoa wa Shinyanga unaendelea kuwa salama na wananchi wanaendelea na shughuli zao za maendeleo bila hofu.

Baadhi ya mafundi walioshiriki semina hiyo wameahidi kuendelea kufanya kazi kwa weledi, uaminifu na kuzingatia maadili ya taaluma huku wakilinda amani ambayo ndiyo msingi wa maendeleo ya sekta ya ujenzi na Taifa kwa ujumla.

Semina hiyo ilihitimishwa kwa burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali wakiwemo mchekeshaji Ndaro, pamoja na TX Dullah, Kidege na Azaboi, ambao wametoa burudani iliyowavutia washiriki wa semina hiyo.

 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Patrobas Katambi, akizungumza na mafundi katika semina iliyoandaliwa na kampuni ya MAGIC BUILDERS mjini Shinyanga

 SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post