
Amesema kwa sasa kuna wimbi kubwa la taarifa potofu zinazosambaa kwa kasi, hivyo ni wajibu wa kila kijana kuwa makini, kufanya utafiti kabla ya kuamini au kusambaza jambo, na kuwa mstari wa mbele kulinda amani na usalama wa taifa kwa kuepuka vitendo vyote vinavyoweza kuhatarisha utulivu wa nchi.
Akizungumza katika Jukwaa la Maendeleo ya Vijana Tanzania linalofanyika jijini Dodoma na kukutanisha jumla ya vijana 600 kutoka mikoa mbalimbali nchini, Naibu Waziri Ayoub amebainisha kuwa dunia ya sasa inakabiliwa na changamoto mbalimbali za kiusalama zikiwemo migogoro ya kijamii na mivutano ya kisiasa.
Ameongeza kuwa matumizi mabaya ya teknolojia na mitandao ya kijamii ndiyo yanayochochea kwa kiasi kikubwa changamoto hizo, hali inayotaka umakini wa hali ya juu kutoka kwa nguvukazi hiyo ya taifa ili kuzuia mifarakano katika jamii.
Kiongozi huyo amekumbusha kuwa amani ndiyo msingi mkuu na wa pekee wa maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kisiasa nchini, na bila hiyo hakuna jambo linaloweza kufanikiwa. Kutokana na ukweli huo, amewasihi vijana kote nchini kujenga utamaduni wa kuwa wazalendo wa kweli na kutunza tunu hiyo muhimu ya amani kwa manufaa makubwa ya vizazi vya sasa pamoja na vizazi vijavyo.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
Post a Comment