Wekundu wa Msimbazi, Simba SC, imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo, Mei 21, 2026, katika Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
Mabao ya Simba SC yamefungwa na
Libase Gueye, Anicet Oura, huku bao la Coastal Union likifungwa na Maabad Maulid
Clatous Chama anaendelea kuonyesha ubora akitoa asisti mbili leo nakuwa mchezaji bora wa mechi (MOM) akiandika rekodi ya kubeba tuzo hizo mara tano mfululizo.
Kutokana na matokeo hayo, Simba SC imefikisha pointi 55 na kuendelea kushika nafasi ya kwanza ikiwa imecheza michezo 24. Wapinzani wao, Young Africans SC, wana pointi 54 wakiwa wamecheza michezo 23, huku wakishika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
Post a Comment