Na Mapuli
Kitina Misalaba
Timu ya Nyandolwa
FC, inayoundwa na wachimbaji wa madini kutoka Mgodi wa Wachapa Kazi uliopo
Nyandolwa, imeondolewa katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 baada ya
kufungwa kwa mikwaju ya penati na Bulige FC katika mchezo wa robo fainali
uliochezwa leo katika Uwanja wa Mwabenda, Kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya
ya Shinyanga.
Mchezo huo
uliokuwa na ushindani mkubwa ulimalizika kwa sare ya goli 1-1 ndani ya dakika
90 za kawaida. Bulige FC ndiyo iliyokuwa ya kwanza kupata bao katika kipindi
cha kwanza kabla ya Nyandolwa FC kusawazisha ndani ya kipindi hicho hicho na
kufanya timu hizo kwenda mapumziko zikiwa sare.
Baada ya
dakika 90 kukamilika bila kupatikana mshindi, sheria za mashindano zilimtaka
mshindi kupatikana kwa mikwaju ya penati ambapo Bulige FC ilionyesha utulivu
mkubwa na kufanikiwa kupata penati 5 dhidi ya 4 za Nyandolwa FC.
Matokeo hayo
yamewaacha wengi wakishangazwa kutokana na Nyandolwa FC kuwa miongoni mwa timu
zilizokuwa zikipewa nafasi kubwa ya kufika hatua ya fainali. Tangu kuanza kwa
mashindano hayo, timu hiyo ilikuwa haijaruhusu kufungwa hata goli moja katika
mechi zake zote kabla ya mchezo wa leo.
Kwa ushindi
huo, Bulige FC imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya NIACHEKONA CUP 2026
na sasa inasubiri mshindi wa mchezo wa kesho ili kujua mpinzani wake katika
hatua hiyo muhimu.
Akizungumza
baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya Mashindano, Sambayi Jilya, ametangaza
kuwa mchezo wa kesho utawakutanisha Shilabela FC dhidi ya Kashishi FC katika
robo fainali ya mwisho ya mashindano hayo, mchezo utakaokamilisha timu
zitakazofuzu hatua ya nusu fainali.
Mashindano
ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na Paul Daud Augustino maarufu MC
NIACHEKONA kwa ufadhili wa Shirika la Lushu Foundation, yakilenga kuibua vipaji
vya vijana, kukuza michezo na kuimarisha mshikamano wa jamii.
Kwa huduma za MC, matangazo na ushereheshaji wa matukio mbalimbali, wasiliana na MC NIACHEKONA kupitia namba 0757 267 738.
Kikosi cha Bulige FC na sabu.
Wachezaji wa Nyandolwa FC na Bulige FC wakionyesha ushindani mkubwa kusaka tiketi ya nusu fainali ya NIACHEKONA CUP 2026.
Viongozi wa mashindano na wadau wa michezo wakifuatilia kwa karibu mchezo wa robo fainali wa NIACHEKONA CUP 2026 katika Uwanja wa Mwabenda.
Mashabiki na wananchi waliojitokeza kwa wingi wakifuatilia mchezo wa robo fainali katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026.
Mashabiki na wananchi waliojitokeza kwa wingi wakifuatilia mchezo wa robo fainali katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026.
Mashabiki na wananchi waliojitokeza kwa wingi wakifuatilia mchezo wa robo fainali katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254



























Post a Comment