" KANISA KUU LA MAMA MWENYE HURUMA PAROKIA YA NGOKOLO LAFANYA UCHAGUZI KUPATA VIONGOZI WAPYA

KANISA KUU LA MAMA MWENYE HURUMA PAROKIA YA NGOKOLO LAFANYA UCHAGUZI KUPATA VIONGOZI WAPYA

 Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Halmashauri walei Kanisa kuu la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo, wamemchagua Ndugu Ignatus Banyemaa kuwa Mwenyekiti mpya wa Parokia hiyo.

Banyemaa ambaye pia ni Mweka hazina wa Kamati ya Mawasiliano Jimbo Katoliki Shinyanga, amechaguliwa kupitia uchaguzi uliofanyika Jumamosi tarehe 22.04.2023, katika ukumbi wa Balina English Medium Primary School, uliopo Ndembezi mjini Shinyanga.
Mkutano huo pia umemchagua Mwalimu James Msimbang’ombe ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Mawasiliano Jimbo kuwa Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri walei Parokia ya Ngokolo, ambapo Ndugu Exavery Selekwa amechaguliwa kuwa katibu wa Parokia.
Aidha Bi. Octaviana Kiwone amechaguliwa kuwa Katibu Msaidizi wa Parokia, ambapo Ndugu John Marwa amechaguliwa kwa mara nyingine tena kuwa Mweka hazina wa Parokia hiyo.
Viongozi hao watatumikia nafasi hizo kwa kipindi cha miaka mitatu, kwa mujibu wa Katiba ya Halmashauri Walei.

Post a Comment

Previous Post Next Post